VIONGOZI 5 WA KIDINI WATOWEKA ZANZIBAR - NIJUZE NEWS

Breaking news

Nyumba ya Habari Makini na za Uhakika

Pata Habari Mpya kwa kina Kila muda kutoka kwanye vyanzo vya Uhakika

Mikoani leo

Mikoani leo

Wednesday, February 14, 2018

VIONGOZI 5 WA KIDINI WATOWEKA ZANZIBAR


Image result for picha za misikiti zanzibar
Jumuiya ya Maimamu Zanzibar imesema viongozi watano wa Dini ya Kiislamu wanadaiwa kutoweka katika mazingira ya kutatanisha.  Hii ni kwa mjibu wa tarifa iliotolewa na Naibu katibu Mtendaji wa wa Jumuiaya ya Maimau Zanzibar  Bw. Khamid Yusuf .

Jeshi la Polisi Zanzibar limekana kuwakamata Viongozi hao kwa kusema hawako mikononi mwa Jeshi la Polisi."Msijeanza sema ooh hao Polisi wameanza".’Amefafanua msemaji wa Polisi ambaye hakuweza kufahamika jina lake mara moja.
Polisi wamesisitiza wanachi kutoa msaada wa kuwatafuta wakishirikiana na Polisi.
Viongozi hao ni Miongoni mwa Watu waliokuwa wakikusanya Michango kwajili ya Familia ya Mashehe ambao wapo ndani Gerezani kwa kipindi kirefu.Michango hiyo nikwaajili ya familia zao ziweze kujikimu kimaisha.

Watu hao wamepotea toka Ijumaa iliyopita,hadi leo hawajuilikani walipo.
Familia za waliopotea wametoa taarifa Polisi na Polisi wanasema wanafuatilia lakini hadi leo haijajuilikana wapo wapi.
Jumuiya ya Maimamu ilalaani kitendo cha kupotea viongozi, Wanasiasa sababu wanaamini Tanzania ina Vyombo vya dola ambavyo vipo imara,vina nguvu na uwezo mkubwa.Kitendo cha watu kupotea ni cha kulaani.
Jumuiya ya Maimamu haifurahishiwi na uvunjaji wa sheria wa nchi hii sababu hawajazoea hii hali ya watu kupotea tu bila kujulikana, si taratibu za kisheria wala si taratibu za kibinadamu.

Jumuiya ya Maimamu inaunga mkono kitendo cha kukusanya fedha kwaajili ya kusaidia familia za mashehe bila kujali wametenda kosa la Ugaidi au hawajatenda,kwa sababu sisi tunaangalia familia za mashehe ikiwemo watoto wadogo wanataabika nyumbani bila msaada.Hatuoni kama zile familia za mashehe zinazotaabika kama zina makosa.
Familia zaidi ya 52 za Mashehe waliokamatwa ikiwemo watoto wadogo wanataabika.”Sisi kama Waislam ni jukumu letu kuwasaidia.”


No comments:

Post a Comment

Mikoani leo

Mikoani leo