VIOONGOZI WA ANC WATAKA KUMNG'OA ZUMA MADARAKANI - NIJUZE NEWS

Breaking news

Nyumba ya Habari Makini na za Uhakika

Pata Habari Mpya kwa kina Kila muda kutoka kwanye vyanzo vya Uhakika

Mikoani leo

Mikoani leo

Tuesday, February 6, 2018

VIOONGOZI WA ANC WATAKA KUMNG'OA ZUMA MADARAKANI

Image result for picha za Jacob Zuma
Jacob Zuma, Rais wa Afrika Kusini
Viongoz wa chama NAC kinachotawala nchini wamechoshwa na uvumilivu wa Rais  Jacob Zuma waliotarajia kujiuzulu baada ya majadilianoa ya wiki kadhaa sasa.
Hapo jana usiku viongozi wa chama cha ANC walitangaza kwamba wataitisha mkutano wa kiwango cha juu wa kamati ya kitaifa NEC kuondosha mzozo wa kisiasa kwa lazima.
Mkutano huo unaotarajiwa siku ya Jumatano unatafanyika siku moja kabla ya hotuba ya bunge ya kila mwaka anayotarajiwa kuitoa Zuma bungeni.
Matarajio ni kwamba NEC itapiga kura kumuondoa madarakani.
Lakini Zuma anaweza kwenda kinyume na matakwa ya chama. Hilo basi litaweza kuzusha uwezekano mkubwa na ambao haujawahi kufanyika wa wabunge wa ANC kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye.
Kauli ya chama cha ANC iliyotolewa kuhusiana na mkutano huo imesema kuwa, wanakutana kujadili ubadilishanaji madaraka kutoka Rais Zuma kama mwenyekiti wa zamani na sasa Cyril Ramaphosa ambaye ni kiongozi mpya wa chama hicho.
Siku ya jumatatu viongozi wandamizi wa chama hicho walilazimika kuwa na mkutano wa dharula mjini Johannesburg kujadili hatima ya rais Zuma.
Hata hivyo rais Zuma ameshikilia msimamo wake kutokubaliana na shinikizo la kumtaka aachie madaraka.
Mwezi Disemba mwaka jana Ramaphosa alimrithi rais Zuma katika nafasi ya juu ya kukiongoza chama hicho kikongwe barani Afrika.
Rais Zuma amekuwaakiandamwa na kashfa za rushwa, ambapo katika miaka ya hivi karibuni alihusishwa na familia yenye asili ya India ijulikanayo kama Gupta - ambapo inadaiwa alitumia madaraka yake vibaya ili kujinufaisha yeye na washirika wake hao.




No comments:

Post a Comment

Mikoani leo

Mikoani leo